KARIBU SANA

Thursday, February 5, 2009

Lisa na kutoswa na mchumba wake

Miss Tanzania namba 3, 2006, Lisa Jensen, ameweka wazi skendo ya ngono inayomwandama na madai ya kutemwa na mchumba wake kutokana na kurusha roho na msanii wa maigizo nchini Steven Kanumba....
Lisa alimwambia mwandishi wetu jana kwa njia ya simu kuwa habari zote zilizotapakaa mitaani ni za uongo na kusema kuna watu ambao wamepanga kumharibia sifa mbele ya jamii.

“Kuna watu wanatengeneza skendo, wanasema nimeachwa na mchumba wangu, mara nafanya mapenzi na Kanumba, yote hiyo ni kunivunjia heshima, mimi sijaachwa” alisema Lisa.

Kuhusu habari za kutengwa na kanisa lake la Sabato analoabudu kwa sasa alisema:
“mimi nasikia tu mitaani, wanasema sionekani kanisani Mwenge nilikokuwa nasali, kifupi kwa sasa nasali tawi la Mikocheni ambako ni karibu na nyumbani.”

No comments:

Post a Comment