KARIBU SANA

Wednesday, January 14, 2009

Marcio Maximo anafaa Taifa Stars?

KUNA mjadala umezuka kuhusu uwezo wa Kocha wa Taifa Stars, Marcio Maximo kama anafaa kuendelea kuifundisha timu hiyo pale atakapomaliza mkataba wake Juni, 2009 au la.

Wanaopinga wanadai Maximo ameshindwa kuweka programu inayoeleweka ya soka kwa miaka mitano ijayo, kushindwa kuiwezesha Tanzania kufuzu katika michuano iliyo mikubwa zaidi na kutoiweka soka ya Tanzania katika ramani inayoeleweka, wengi wanadai kazi hiyo heri apewe Kocha wa Vijana, Tinoco.

Wanaomtetea wanadai Maximo amefanikiwa kutokana na kuiwezesha Tanzania kwenda katika Mashindano ya CHAN, Ivory Coast pamoja na kuiweka Tanzania katika ramani ya soka kuliko huko nyuma.

Mtazamo wako ni upi? Je, Marcio Maximo anafaa au hafai?

Matokeo ya maoni hayo yatachapishwa pia katika gazeti la Championi Ijumaa

No comments:

Post a Comment