KARIBU SANA

Tuesday, February 24, 2009

BREAKING NEWS .....!!!!!LIYUMBA AJISALIMISHA!!!

Hatimaye aliyekuwa Mkurugenzi wa Utawala wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Amatusi Liyumba leo amejisalimisha katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kisha kufutiwa dhamana yake na kutupwa lumande.

Liyumba ambaye alitoweka wiki moja iliyopita na kutolewa hati ya kusakwa kwake huku donge nono likitangazwa kwa mtu yeyote ambaye angefanikisha kukamatwa kwake, alitinga katika mahakama ya Kisutu majira ya saa 3 asubuhi akiwa kwenye gari aina ya Lite Ace lenye namba za usajili T 526 AVB akiwa na wakili wake Majura Magafu.

Baada ya kutua huku akilakiwa na umati mkubwa wa watu, Liyumba aliingia katika ofisi ya waendesha mashitaka ambapo baadaye alitolewqa akiwa chini ya ulinzi na kutupwa Selo kabla ya kupandishwa kizimbani akiwa sambamba na mtuhumiwa mwenzake Kweka.

Wakili wa upande wa mashtaka Prosper Mwangamila aliiomba mahakama kumfutia dhamana Liyumba kwa kuwa alikuka masharti na kwamba tayari hati ya kudakwa kwake ilikuwa imetolewa na imetekelezwa.

Hoja hiyo ilifafanuliwa zaidi na Hakimu anayeendesha kesi hiyo Bi.Khadija Msongo ambaye alidai kuwa Mahakama yake ndiyo iliyotoa hati ya kukamatwa kwa Liyumba baada ya kubaini kuwa aliwasilisha mahakamani hapo Pasport iliyokwisha muda wake huku akiondoka na Passporti hai.

Hata hivyo hoja hiyo ilipingwa vikali na wakili wa Liyumba Majura Magafu, ambaye alikili kuwa mteja wake aliwasilisha Passpoti hiyo kwa bahati mbaya.

Hoja hiyo ya Magafu, ilitupiliwa mbali na Mahakama, ambayo baadaye ilitangaza kumfutia dhamana Liyumba huku ikidai kuwa pamoja na kuidanganya mahakama kwa kuwasilisha Pasport iliyo 'Expire' lakini pia hati zake zote 10 za dhamana alizowasilisha mahakamani hapo zenye thamani ya Shiligi Milioni 800 ni batili

Hakimu Msongo alimtupa tena ndani Liyumba hadi Machi 10 ili aweze kutimiza masharti ya dhamana.

Hebu fuatilia matukio haya yafuatayo ujionee jinsi picha lilivyo kuwa mahakamani Kisutu leo.
Liyumba (mwenye shati la bluu) akiwa ameshuka kwenye gari mapema asubuhi.
Liyumba akiingia katika mahakama ya Kisutu leo, kushoto ni wakili wake Majura Magafu.
Huu ndiyo mkoko aliyotinga nao mahakamani hapo.
Mapaparazi wakimsubiri kwa hamu kabla ya kuingia mahakamani.
Liyumba akitolewa kizimbani baada ya mahakama kuamuru atupwe lupango.
Liyumba akiagana na baadhi ya jamaa zake huku akiwa chini ya ulinzi mkali tayari kwa kurejeshwa lupango
Hapa akichukisindikizwa kwenda Mahabusu Mahakamani hapo.
Akiingia kwenye basi la Magereza tayari kwenda Magereza ya Keko.
Ndugu na jamaa wakimpungia mikono.
Safari ya Keko ilianza.

No comments:

Post a Comment